JINSI YA KUWEKA PASSWORD KWENYE DOCUMENT YAKO

 

JINSI YA KULINDA DOCUMENT YAKO.

Watu wengi huwa tunahifadhi vitu vingi kwenye mfumo wa PDF lakini bado kila mtu akiigusa tu document yako anajua nini ulichokiweka.



Usiogope ni rahisi sana tena Zaidi ya sana na unaweza kulifanya hili kupitia kompyuta yako au kifaa chochote amabacho kinasupport PDF readers zenye uwezesho wa Ulinzi (protection)


PDF READERS NZURI KWA KAZI HII

Kuna PDF readers nyingi sana ambazo zipo na watu wengi wanazitumia PDF reader hizo ili kufungua na kuzisoma Pdf file ambazo wanazo. Sasa kwa hapa nakufundisha kuhusu aina mbili za PDF readers ambazo ndizo mara nyingi huwa nazitumia na zinafanya kazi kubwa hata ya kuedit PDF, ni maajabu lakini ujue pia PDF inaweza kueditiwa vizuri na ukaiongezea kitu au ukapunguza kitu, kwahiyo tunaenda kujifunza tu namna gani ya kuweka PIN/PASSWORD kwenye document yako.

PDF reader hizo ni

i.                    PDF ETRA

ii.                  ADOBE READER

Hizi ndizo Pdf reader ambazo nazozitumia na zinafanya vizuri sana hususani katika kufungua PDF na kuedit pia PDF hususani PDF EXTRA ndio Bora Zaidi ukilinganisha na ADOBE READER.

Pasipokuchelewa twende moja kwa moja kuona hatua ambazo unatakiwa kuzifuata ili uweke ulinzi kwenye PDF yako

 HATUA ZA KUFUATA KUWEKA PIN/PASSWORD KWENYE PDF YAKO.

1.     Hakikisha una PDF EXTRA na umeinstall kwenye Computer yako.

Hujui ni mahali gani pa kuipata program hii, usiogope utabonyeza link ili kuidownload na ukainstal kwenye PC au komputa yakp.

2.     Hakikisha document yako ipo kwenye PDF



ili uweze kuiweka kwenye mfumo wa kulindwa, kama huwezi kuweka Documents kwenye mfumo wa pdf basi endelea kuwepo name nitakufundisha namna gani ya kufanya ili uweke kwenye mfumo wa PDF au fuatilia video zetu youtube https://youtube.com/@technoonlineriches

3.     Ifungue Pdf file yako kwa kutumia PDF EXTRA kisha fuata hatua hizi zinazofuata

4.     Bonyeza mahali pameandikwa PROTECT



5.     Bonyeza palipoandikwa PROTECT DOCUMENT



6.     Baada kubonyeza hapo utaletewa ujumbe unaosema “changing the password requires the file to be saved. You will not be able to undo/redo after this operation” na ikiwa imeambatana na chaguo mbili, basi wewe bonyeza OK



7.     Itafunguka kuraza ya USER RIGHTS hapo basi utatakiwa ujaze kwa mfumo unaoutaka.

Chaguo zipo katika sehemu 3 ambazo ni

i.                    OPEN SOCUMENT

ii.                  PERMISION

iii.               ENCRYPTION

I.                   OPEN DOCUMENT

Sehemu hii ni ya kwanza kabisa ambayo yenyewe inahusiana na swala la kufungua tu document, maana yake ni kwamba, ukiweka password kwenye sehemu hii basi hakuna mtu atakayeweza kufungua document hii hadi aijue password ya kufunguliA

ILI KUPATUMIA

·        Utaweka alama ya Tick kwenye box

·        Utaweka password yako

·        Utairudia password yako

·        Kisha bonyeza OK hapa utabonyeza ok kama nia yako nikuishia hapo ila kama unataka kwenda Zaidi basi utaenda kwa hatua ya pi.



II.                 PERMISSION

Mahali hapa unaenda kubase na vitu unavyotaka kuviruhusu au kutokuviruhusu kwenye document yako mfano kueditiwa, kuprintiwa au kufanyiwa kitu chochote, na hapa unaweza kuweka password yoyote kama ukiamua kutumia uliyoitumia kwenye kufungua au ukaunda mpya tofauti na ile uliyoiweka mwanzo.

JINSI YA KUWEKA ULINZI MAHALI HAPA

·        Weka alama ya Tick kwenye kibox

·        Weka password alafu irudie tena kwenye sehemu ya chini yake

·        Kisha bonyeza neon OK hapo tayari utakuwa umeiaset, kwan hakuna atakaye kopi wala kuprint document yako bila password.




ZINGATIA

Baada ya kuweka ulinzi kwenye document yako jambo la kuzingatia ni kwamba hautakiwi kusahau password uliyoitumia kwenye document yako, ukishaisahau basi hauna nafasi ya kuipata tena hiyo document yako.

Kwanini?

            Kwasababu hakuna chaguo la kurecover password yako, kwahiyo hakikisha unaweka password ambayo utaikumbuka au hakikisha unaiandika mahali ili kutunza kumbukumbu ya password yako.

 


Ni furaha yangu kwamba nimeeleweka vizuri na utafanya vizuri katika kuendelea kutunza mali zako, document zako mbali mbali. Uzuri wa hii ni kwamba hakuna mtu atakayeweza kuitumia isipokuwa umempatia password yako.

 Kulinda taarifa na mali zako ni wajibu wako. Na hii ni mbinu ya kuzitunza mali zako.

Ahsante na majukumu mema

By

             Thobias Cosmas (Caza Von Th)

About TECHNO ONLINE RICHES

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment