KWANINI MASIKINI HUCHELEWA KUFIKIA UTAJIRI?

 


KWANINI MASIKINI HUCHELEWA KUFIKIA UTAJIRI?

Bado kunachangamoto kubwa kwa masikini kuuendea utajiri, na mara zote masikini huwa anachelewa sana kuuendea utajiri. Na hii inatokana na sababu mbali mbali.

MASIKINI NI NANI?

Masikini ni mtu yeyote yule asiye na maendeleo ya kiuchumi yaani hawezi kukidhi mahitaji yake yote kama chakula, malazi na Makazi pia.

Masikini wengi hawawezi kufikia mafanikio yao kiurahisi kwasababu ya changamoto nyingi ambazo wanazozipitia kuelekea mafanikio. Kuna msemo unaosema “MWENYE VINGI HUONGEZEWA” msemo huu unauelewa vipi? Msemo huu una maana kubwa sana kimsingi, maana yake kwamba mtu ambaye anacho kitu basi anaweza kuongezewa ili afanye bora Zaidi ila mtu asiye na kitu basi hakuna haja ya kumpatia chochote ila tu atanyang’anywa na kidogo alicho nacho.

NI MCHAKATO wa muda mrefu masikini kuufikia utajiri, ila ni mchakato wa muda mfupi sana tajiri kuufikia umasikini endapo akishindwa kuwa na akili ya kutunza utajiri alionao,

Unadhani ni kwanini masikini wengi huwa ni vigumu kuufikia utajiri.

SABABU ZA MASIKINI WENGI KUCHELEWA KUFIKIA UTAJIRI

Zifuatazo ni sababu kuu zinazosababisha masikini wengi kuchelewa kuwa matajiri.

1.      1. Kukosa msaada wa kifedha kwenye ndoto zao (Lack of financial support)

2.       2. Kukosa watu sahihi katika njia za mafanikio yao (lack right people in their plan)

3.       3. Kukosa Imani ya mafanikio (give up on their goals)

4.       4. Kuridhika na hali zao (satisfaction)

5.       5. Kukosa elimu ya uwekezaji na kujitegemea (lack of education of investment and self-reliance)

6.       6. Mizigo mingi ya tegemezi (large number of dependants)

 

 

1.       1. Kukosa msaada wa kifedha kwenye ndoto zao (Lack of financial support)

Furaha yangu ni kueleweka juu ya hili jambo, miongoni mwa watu wanaopambana sana huwa ni masikini, na lengo kubwa nikujikwamua kutoka kwenye wimbi kubwa la umasikini. Tatizo kubwa ni kwamba waliowengi

Ubaya Zaidi ni kwamba mtu anaweza kuwa na ndoto Fulani na hiyo ndoto ni kubwa ambayo mtu yeyote akiifanya anaweza akafanikiwa sana, lakini ugumu unakuja kwamba “upele umemuota asiye na kucha.” Mara nyingi masikini huwa wanamawazo mazuri na mbinu nyingi za kibiashara lakini ubaya unakuja sehemu moja kwamba wanashindwa kufikia zile ndoto zao kwasababu wanakosa misaada ya kifedha kuelekea ndoto zao.

Ukosekanaji wa misaada ya kifedha imekuwa ni sababu kubwa ya masikini kuchelewa kufikia utajiri maana muda mwingi huutumia kutafuta pesa kwa njia zingine ili kufata malengo yake yaliyo katika njia zingine, hii ndio sababu kubwa ya Masikini Wengi Kuwa Na Vitu Vingi Wanavyoweza Kufanya.

2.       2. Kukosa watu sahihi katika njia za mafanikio yao (lack right people in their plan)

Natamani kulielezea hili katika huzunu kubwa. Siku zote ndege wafananao ndio huruka pamoja. Kwanini?, ni kwasababu wanaongea lugha moja.

Rafiki wa masikini mkubwa huwa ni masikini mwenzake na rafiki wa tajiri mkubwa huwa ni tajiri mwenzake, unadhani ni kwanini? Ni kwasababu Tajiri wengi huamini kwamba masikini akiwa naye karibu hana akili ya kumuwezesha yeye kujenga mafanikio, isipokuwa ni watu waliojaa shida shida na kulia lia mbele zao wakitafuta msaada. Kitu kichi kinapelekea matajiri kujitenga na masikini na hatimae masikini kuishi katika maisha ya kimasikini na marafiki wa kimasikini.

Kwanini hili swala la kukosa watu sahihi ni tatizo, ni kwamba, ili kupata millioni kutoka kwenye kipato cha elfu maana yake ukutane na akili za mamilioni ambazo hizi unazipata kwa mtu mwenye mawazo ya mamilion. Kama unataka kupiga hatu hiyo usipopata mtu mwenye akili hiyo maana yake ni kwamba hautaweza kufikia millions utaishia elfu tu.

Watu wanaokuzunguka wakiwa sahihi na kuendana na kile unachokiwaza inawezekana ukakifikia na ukafanikiwa.

Rafiki wa masikini ni Masikini mwenzi hii ndio shida.

 

3.       3. Kukosa Imani ya mafanikio (give up on their goals)

Mara nyingi masikini wengi hukosa Imani ya wao kuja kuwa matajiri, kwasababu hufikia kusema “Babu alikuwa masikini, mama na baba walikuwa masikini, ndugu zangu masikini, Nitatoboa kweli, mbona wao walishindwa?!, hapa siwezi kutoboa  mitazamo inayojengeka kwa wengi ni kwamba kama familia au ukoo wake ni masikini basi anaamini na yeye kuwa masikini ni kanunu za ukoo na hatimae mtu hukata tamaa na kushindwa kuendelea kupambana. Hili ni tatizo.

Pia wengine hukata tamaa baada ya kuona kila wanachokipanga hakina majibu kwao baada ya kukosa msaada wa kifedha na watu sahihi kwenye safari yake ya upambanaji. Inauma sana kuongea hili lakini lazima watu waelewe kwamba kukata tamaa kunasababisha wtu waliowengi kuchelewa kufikia utajiri na hatimae baadhi hufa masikini. Kwanini unakata tamaa, kwasababu umeona kizuizi usichoweza kukivuka, kwanini huwezi kukivuka, kwasababu umeaminishwa hivyo ndani yako. Pole sana, unajichelewesha, amini kila kitu kinawezekana.

 

4.       4. Kuridhika na hali zao (satisfaction)

Huwa nasikitika sana juu ya jambo hili lakini ndilo lililopo kwa watu wengi sana, sasa twende sawa nilielezee hili. Swala la kuridhika sio dhambi ila swala la kulidhika penye hamna hii ina maana kwamba huelewi umeridhika na kitu gani. Utamkuta masikini anasema “nimeridhika na hali yangu” mimi binafsi huwa nikimsikia mtu anatoa kauli hii namuita mpumbavu asiye na akili kabisa kwasababu hakuna mtu anayeridhishwa na kukosa mahitaji yake. Kuridhika na hali kunampelekea mtu kuwa mvivu na kushindwa kufanya kazi za kuendelea kutafuta pesa.

Pesa ni kitu kinachotafutwa endelevu, yaani hakuna mwisho wa kutafuta pesa labda uwe umekufa, lakini kama upo hai basi huwezi kuridhika na pesa ulizonazo lazima uendelee kutafuta pesa ili uwe na uhakika wa mzunguko wake. Usiridhike na Umasikini, utajikuta unahama kwenye umasikini unaanza kuwa FUKARA. Ukiridhika kwenye umri wa miaka 15 – 50 maana yake ni kwamba miaka 60 hadi kifo utakuwa FUKARA sio masikini isipokuwa masikini aliye bobea umasikini. Hii sio sifa, TASAF imekuja kwa niaba ya masikini sasa kama TASAF itakutosha acha kufanya kazi.

 

5.       5. Kukosa elimu ya uwekezaji na kujitegemea (lack of education of investment and self-reliance)

Baadhi ya watu wanachelewa kufikia utajiri kwasababu ya kukosa elimu ya uwekezaji kwa kidogo walichonacho, elimu ni swala la msingi kutolewa kwa masikini juu ya namna gani wanavyoweza kufanya uwekezaji kwa kidogo wanachokipata. Elimu ya uwekezaji inahitajika sana kwa masikini. Najua kuwa hata masikini awe vipi hawezi kushindwa kupata hata elfu 50 kama ataweza kuipata hata kwa miezi 5 je, umewahi kuwaza namna gani unaweza kuizalisha hiyo, kama hapana basi endelea kujifunza kupitia blog hii utapata elimu kubwa sana kuelekea mafanikio yako. Jifunze kuwekeza ili uweze kufanikiwa.

 

6.       6.BMizigo mingi ya tegemezi (large number of dependents)

Hii ni tatizo kubwa ambalo linawakumba 99% ya wapambanaji ndani ya familia za kimasikini. Shida kubwa ni kwamba mtu huyu anyechukua muda mwingi kutafuta pesa, basi wapo watu wengi ambao wanamtazama wote wakihitaji kupokea msaada kupitia huyo huyo mtu mmoja, mlundikano wa mizigo mingi tegemezi kwenye familia hupelekea wengi kuishia umasikini na hata kutikuuonja utajiri, kwasababu kila wanachokipata kinapitiliza moja kwa moja kwenye matumizi na kuzisaidia familia.

Maisha tegemezi yanapelekea vijana wengi kufa masikini hususani waliotokea katika familia za kimasikini. Ili kutoboa hapa ndipo panapoleta changamoto kubwa katika mwelekeo mafanikio.

 

HITIMISHO

Hivi vitu vimekuwa changamoto kubwa kuelekea utajiri kutokea umasikini, ila njia pekee ya kufanya mabadiliko ni kujua ni mbinu gani za kufanya ili kujitoa kwenye hivyo vikwazo ili ufike katika hatua ambayo unaweza kuifikia.

Kila mtu anaweza kuwa tajiri ila tu chamsingi ni kujua namna gani ya kujitoa kwenye misingi ya kimasikini na kutembea jatika misingi mipya ya utajiri.

 

Nifuraha yangu kuwa umeelewa, na kama unaswali basi uliza kwenye comment box hapo chini name nitakujibu kwa wakati, shukrani sana.

                                        Thobias Cosmas (caza vin Th)

About TECHNO ONLINE RICHES

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment