JINSI YA KUJIWEKEA MALENGO KWENYE MAISHA YAKO.
MALENGO:
Ni
mipango au dhima au matamanio ya mtu aliyonayo juu kupata matokeo Fulani,
malengo yanapozungumziwa mara nyingi hulenga kuangalia ndoto za mtu au shauku
aliyonayo mtu. Na malengo hapa tunazungumzia malengo katika uchumi, malengo
ambayo yanaweza kukusaidia kuwa mwongozo wa wewe kuelekea mafanikio yako ya
kiuchumi, kwasababu malengo ni njia kuelekea mafanikio.
Mafanikio:
Mafanikio
ni hatua mtu anayopiga kutoka katika hali ya chini hadi hali ya juu ambapo
tunaweza kusema mafanikio ni sawa na maendeleo. Mafanikio hayaji yaji tu,
hapana, mafanikio yanatengenezwa hatua mpaka hatua na katika hatua kuelekea
mfanikio basi lazima uzifuate, huwezi kufikia mafanikio kama hufuati hatua
zinazokuongoza hadi kuyafikia mafanikio yako
Jifunze hatua kuelekea za
mafanikio
Katika kelekea mafanikio lazima ukubali kujitoa kwa nguvu
katika kuandaa malengo ambayo pia yananguvu na yanafuata kanuni za kuweka
malengo.
Malengo Mazuri na yanayotambulika huwa yanafuata kanunu, na
zifuatazo ni kanuni na sifa za malengo
KANUNI / SIFA ZA
MALENGO (SMART PLANS)
Malengo kwa kawaida yanatakiwa kuwa na sifa zisizopungua
tano ambazo ni
1.
Malengo yawe Maalum (SPECIFIC)
2.
Malengo yaweze Kupimika (MEASURABLE)
3.
Malengo yawe Yanafikika (ATTAINABLE)
4.
Malengo yawe Halisi (REAL)
5.
Malengo yawe na muda unaoeleweka (Time Frame)
UFAFANUZI WA KANUNI
1. MALENGO YAWE MAALUM (SPECIFIC)
Malengo maalum ni malengo ambayo yanaeleweka na
yanatambulika vizuri (Clear and identified), ni malengo ambayo hata wewe uliye
yaandika utayaelewa kwamba yanataka nini, ukiwa unaandaa malengo hakisha
unazingatia swala la kuelweka kwa malengo yako, Malengo smart ni malengo ambayo
lazima yawe wazi na kutambulika, usiandike malengo kwa mafumbo ili mwingine
asielewe la hasha unapoandika kitu kwa mafumbo umejipa kazi hata wewe kutafuta
maana ya mafumbo hayo. Malengo mazuri ni yale yaliyo wazi na kueleweka, yaani
wewe mwenyewe unayaelewa vizuri.
Kutengeneza malengo wazi yanahitaji pia utuvu wa namna ya
kuandika, malengo wazi ni sawa na uandishi kwa kichwa cha habari au kichwa
kidogo cha habari (Title/subtitle)
Mfano: kama unataka gari andika Gari RAV4 au Kununua gari
RAV4
Sio
kuandika maelezo, yani mwaka huu nataka nikifanikiwa tu nipate pesa ili nione
namna ya kununua gari tena RAV4 hii ni unyama sana.
Hii sio lengo, hii ni vurugu ya lengo, kwahiyo lengo
liandikwe vizuri na lieleweke vyema.
2. MALENGO YAWEZE KUPIMIKA (MEASURABLE)
Ni kweli kabisa malengo mazuri ni yale yanayopimika,
yanayoweza kupimwa yaani kuchunguzika katika mzani kwamba linawezekana au
haliwezekani. Lengo likiwa linapimika maana yake linaweza kuingia kwenye
kuchakatwa na kuonekana namna gani linaweza kutimizwa, lakini pia lengo likiwa
lenye kupimika maana yake unaweza kulilinganisha lengo hilo na malengo mengine hii
itakusaidia kufanya maamuzi ya lengo gani la kutembea nalo, au kuanza nalo na
kuyaweka malengo yako yote katika mpangilio.
Kiufupi, malengo kupimika maana yake ni kupima uzito wa
lengo hususani kwenye matokeo yake baada ya kufanikiwa, pia umuhimu wake na
namna inavyogharimu ili kulifikia, kwahiyo lengo zuri linapimika.
3. MALENGO YAWE YANAFIKIKA (ATTAINABLE)
Ndio, malengo yanatakiwa kuwa na uwezekano, yani yawezekane
kutimia au kufikiwa, ukipanga malengo ambayo huwezi kuyafikia maana yake ni
kwamba hauna kazi unayoifanya isipokuwa unapoteza muda tu, malengo mazuri ni
yale yanayofikika na mtu anaweza kuyatimiza.
Malengo yasiyofikika ni malengo ambayo yanamuda mrefu sana
Zaidi ya umri na vyanzo vya kipato
Mfano: Unafanya biashara ya kuuza nyanya na unaweka malengo
ya kusema utanunua ndege. Je, kweli utafikia lengo hili? Jibu ni hapana sio
rahisi kulifikia kwa maana hiyo umeweka lengo ambalo halifikiki
HESABU NDOGO
Nyanya mtaji ni Tsh. 200,000/=
Faida kwa mwezi ni Tsh. 200,000/=
Kwa mwaka = 200,000 x 12 = 2,400,000/= hapa hujatumia kwa
matumizi yoyote
Ndege inathamani mfano wa Tsh. billioni 1 = 1,000,000,000/=
Hii utaitimiza kwa muda miaka mingapi 1,000,000,000 ÷
2,400,000 = 416.67 yaani kutimiza bilioni moja unahitaji miaka 416.67 ili uweze
kununua ndege. Kwa lugha rahisi ni kwamba Malengo yako ni batili yasiyofikika.
Hapa nadhani nimeeleweka vizuri.
Malengo yawe yanayofikika na hapa utaweza kufanikiwa sana.
4. MALENGO YAWE HALISI (REAL)
Malengo yawe halisi. rafiki, ukipanga malengo yasiyo na
uhalisia ni sawa na kupoteza muda, malengo yanatakiwa yawe halisi bana,
yanayoonekana na kuwezekana, kwasababu malengo halisi yanayonjia halisi pia ya
kuyaendea, usweke malengo kama “Kuumba mtu, Kutengeneza ndege, kutawala Dunia.”
Hapa utakuwa unapoteza muda yani hauna kazi ya kufanya, swala la malengo lazima
yawe halisi kuendana na mazingira, kipato na waliasili zinazokuzunguka, ili
kuweka malengo halisi lazima uzingatia vile vilivyopo vinavyopatikana na
kuwezekana kisha weka malengo yako.
5. MALENGO YAWE NA MUDA UNAOELEWEKA (TIMEFRAME)
Malengo bila muda maalumu ni sawa
na kutembea safari usiyoelewa unafika lini. Safari usiyoielewa inaisha lini ni
bora tu kutokuifanya, maana inawezekana ikawa safari ya miaka 100 na ukajikuta
unapoteza maisha na safari bado hujaimaliza. Unapoweka malengo hakikisha
unayawekea na muda, usipoyawekea muda hayana maana kuwepo, hii ndio maana
halisi ya mkataba. Malengo ni kama mkataba una muda maalum, mkataba usio na
muda maana yake hauna mwisho, sasa ukiweka lengo la hivi sio lako hilo achana
nalo. Unapotaka kuweka lengo hakikisha unaliwekea muda maalum baada ya kujua
kwamba linafikika basi liwekee muda utalifikia lini. Lengo zuri linaongozwa na
muda uliowekwa kuelekea lengo hilo.
HITIMISHO
Malengo mazuri yanatimia, na hata
kama utakutana na changamoto nyingi lakini yanatimia, jambo la msingi ni
kuhakikisha hutoi mwanya wa mtu yeyote kuzimisha malengo yako uliyojiwekea na
hapa utaweza kufikia kile ambacho unatarajia kufikia kwa wakati husika. Najua
unajua kwamba malengo ni mafanikio, mafanikio ni malengo, hakuna mtu yeyote
aliyefanikiwa pasipo malengo.
Kwahiyo Weka malengo smart kwa
kuhakikisha kuwa malengo yako yanaeleweka, yanaweza kupimika/ kulinganishwa
vizuri na kuchakatwa, malengo yako yanaweza kufikiwa, malengo yako ni halisi na
yenye muda maalumu wa utimilizwaji. Ukifanikiwa hapa lazima utatembea vizuri
kwenye safari ya mafanikio.
Ahsante sana kwa kujifunza. Kama
utakua na swali la aina yoyote basi unawezaa kuuliza hapo chini na nitakurudia
ili kukupatia majibu kwa wakati, ahsante na endelea kutufuatilia.
Imeandikwa na
Thobias Cosmas au Caza Von Th.
Ahsante mwalimu kwa darasa zuri, najifunza kwako
ReplyDelete